Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akisaini Kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo mara baada ya kuwasili katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu Jijini Dar es Salaam, tarehe 27 Februari, 2026.